Waziri wa Afya nchini Kenya Mutahi kagwe amesema kuwa leo Jumatatu kutafanyika mkutano wa dharura kujadiliana ongezeko la maambukizi ya ugonjwa wa Covid-19 nchini humo sio tu kwa raia wa kawaida bali hata kwa wahudumu wa afya.
Hatua hiyo inajiri huku Chama cha Madaktari nchini Kenya kikitoa ilani kwa serikali ya mgomo wa siku 21 baada ya wahudumu wa afya wapatao 10 kupoteza maisha katika kipindi cha siku nne zilizopita kwasababu ya virusi vya corona.
Madaktari wanashutumu serikali kwa kuhatarisha maisha yao.
Ijumaa wiki iliyopita madaktari wanne walifariki dunia siku hiyo ingawa bado haijajulikana kama walikuwa wamekutana na wagonjwa wenye maambukizi ya virusi vya corona.
Kaimu katibu wa chama cha madaktari Mwachonda Chibanzi, amesema kuwa hawatasitisha mgomo huo hadi matakwa yao yatakapotimizwa.

No comments:
Post a Comment