Search This Blog

Monday, November 16, 2020

Afrika Kusini yataka muhubiri milionea aliyetorokea Malawi arejeshwe


Serikali ya Afrika Kusini imesema kuwa imewasiliana na Malawi ili ikabidhiwe muhubiri mtata, Shepherd Bushiri, na mke wake Mary, baada ya wanandoa hao kuvunja masharti ya dhamana.

Wawili hao wanakabiliwa na makosa ya udanganyifu na utakatishaji wa fedha nchini Afrika Kusini.

Bwana Bushiri, kiongozi wa Kanisa la Enlightenment Christian Gathering Church, ambaye pia anafahamika na wafuasi wake kama Major 1, alitangaza Jumamosi kwamba ametoroka Afrika Kusini baada ya kupokea vitisho vya kuuawa.

Aidha, alikataa kuelezea wazi BBC namna alivyofanikiwa kutoroka lakini inakisiwa kuwa walipita mpakani kwa njia ya magendo kwa usaidizi wa genge linalohusika na uuzaji wa magari yalioibwa.

Kutoroka kwake kumechochea mazungumzo ya kidiplomasia kati ya Afrika Kusini na Malawi.

Serikali ya Afrika Kusini imewataja wanandoa hao kamawatoro ambao ni lazima wakabidhiwe nchi hiyo ili kukabiliana na mkono wa sheria.

Rais wa Malawi Lazarus Chakwera ambaye alikuwa Afrika Kusini kwa ziara rasmi wiki iliyopita, alishtumiwa kwa kumsaidia Bwana Bushiri kutoroka – madai ambayo ameyakanusha.

Pia serikali ya Afrika Kusini imethibitisha kuwa mhubiri huyo milionea nchini Malawi, hakutoroka kwa kutumia ndege ya rais.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...