Search This Blog

Friday, November 20, 2020

Malawi yamuachia huru Nabii milionea aliyekiuka masharti ya dhamana Afrika Kusini


Nabii milionea wa Malawi Shepherd Bushiri na mke wake wameachiwa bila masharti yoyote na mahakama moja mjini Lilongwe nchini Malawi baada ya kujisalimisha kwa polisi Jumatano.

Afrika Kusini inataka ikabidhiwe wawili hao kwa kukiuka masharti ya dhamani nchini humo.

Bushiri na mke wake wameshtakiwa nchini Afrika Kusini walikokuwa wanaishi kwa makosa ya utakatishaji wa fedha na ulaghai.

Hata hivyo wawili hao wamekanusha mashtaka hayo.

Wakili wao, Wapona Kita, aliitaka mahakama iwaachilie wawili hao bila masharti yoyote akisema kuwa kukamatwa kwao ni kinyume na sheria.

Mwendesha mashtaka aliomba mahakama kuruhusu polisi kuendelea kuwashikilia wanandoa hao kwa siku 30 zaidi ili kuwezesha Afrika Kusini kuwasilisha rasmi ombi lao la kutaka wakabidhiwe kwa nchi hiyo.

Bwana Kita alisema ni kinyume cha sheria kumzuilia mtu wakati Afrika Kusini haijawasilisha ombi rasmi.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...