Search This Blog

Monday, August 10, 2020

Mr kuku kizimbani kwa kufanya biashara haramu ya upatu na uhujumu uchumi

Mfanyabiashara, Tariq Machibya (29) maarufu kama Mr. Kuku, amefikishwa Mahakama ya Kisutu, akikabiliwa na mashtaka 7 likiwemo la kufanya biashara haramu ya upatu kwa kukusanya fedha za Umma zaidi ya Tsh. Bilioni 17

Machibya amesomewa mashtaka yake leo 10/08/2020 na Wakili Mwandamizi wa Jamhuri, Simon Wankyo mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Godfrey Isaya

Mbali na shtaka la kusimamia biashara hiyo haramu ya Upatu, Mr. Kuku anayekabilia na Kesi ya Uhujumu Uchumi pia ana mashtaka ya Kupokea maingizo ya fedha kutoka kwa Umma bila leseni na kutakatisha fedha

Anatuhumiwa kupokea maingizo ya fedha kutoka kwa Umma akiwadanganya kuwa watafanya Ujasiriamali wa ufugaji wa kuku na watapata faida ya asilimia 70 kwa waliowekeza kwa miezi 8 na asilimia 90 kwa waliowekeza kwa miezi 6, kiasi kinachoelezwa kuwa kikubwa kuliko mtaji uliokusanywa

Pia, kati ya Aprili 26, 2019 na Januari 26, 2020 jijini Dar anadaiwa kujihusisha na miamala ya Tsh. Bilioni 6.4 kutoa katika akaunti iliyoitwa Mr. Kuku Pharmacy katika Benki ya CRDB huku akijua fedha hizo ni zao tangulizi la biashara haramu ya Upatu

Aidha, anadaiwa kupokea fedha kiasi cha Tsh. Bilioni 17 ya maingizo ya Umma bila kuwa na leseni. Upande wa Mashtaka umesema upelelezi haujakamilika na kesi imeahirishwa hadi Agosti 24, 2020 huku mtuhumiwa akirudi rumande kutokana na makosa hayo kutokuwa na dhamana




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...