Kwa maana hiyo Feisal atakuwa ni mali ya Yanga mpaka 2024 kwa timu itakayokuwa inasaka saini yake lazima ijipange kuweka mkwanja mezani.
Kwa msimu wa 2019/20, Feisal amekuwa bora ndani ya Ligi Kuu Bara akianza kikosi cha Kwanza kwenye jumla ya mechi 22.
Ana tuzo ya mchezaji bora ndani ya Yanga aliyokabidhiwa na wadhamini wakuu wa Klabu hiyo, kampuni ya SportPesa.
Amefunga bao moja ndani ya ligi msimu huu ilikuwa Uwanja wa Mkapa dhidi ya Mwadui FC kwenye sare ya kufungana bao 1-1.
No comments:
Post a Comment