Search This Blog
Wednesday, July 22, 2020
Wakulima zaidi ya mia nne kulipwa fedha zao za Korosho Mkoani Mtwara
Na Faruku Ngonyani , Mtwara
Wakulima Zaidi ya Mia Nne (400) wa zao la korosho waliokuwa wadai fedha zao kwa msimu wa 2019/2020 Mkoani Mtwara kulipwa ndani ya wiki hii.
Hayo yamethibitishwa na Mkurugenzi wa benki ya Maendelendeo ya Kilimo Tanzania Japhet Justin alipokuwa anazungumza na wakuu wa idara za Halmashauri ya Manispaa Mtwara Mikindani Pamoja na Halmashuri ya Wilaya ya Mtwara.
Mkurugenzi huyo amesema kuwa kwa Mkoa wa Mtwara wakulima wanadai bilioni 12 huku Wilaya ya Tandahimba kuna deni la bilioni 9,Wilaya ya Mtwara Milioni 844 na Wilaya ya masasi bilioni mbili (2).
Awali madeni ya wakulima kwa Mkoa mzima wa Mtwara yalikuwa Bilioni Mia nne na Moja (401) .
Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo ameeleza mpaka kufika siku ya Juma mosi tarehe 25 julai 2020 wakulima kwa kiasi kikubwa watakuwa wamepata fedha zao: ”haya madeni yote yanakwenda kuondoka na nina uhakika hizi siku zinavyozidi kwenda mpaka kufikia juma mosi mpaka ya ijayo haya madeni yote yatakuwa yamelipwa”
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment