Bunge la Zambia limelazimika kufungwa baada ya Msajili wa Bunge, Rogers Mwewa kufariki baada ya kupata maambukizi ya Corona Virus
Mwewa alifariki na kuzikwa Julai 21. Makamu wa Rais, Inonge Wina amesema kutokana na kuongezeka kwa kasi ya maambukizi ya #COVID19 wamelazimika kuahirisha Bunge
Spika wa Bunge la Zambia, Patrick Matibini ataongoza katika zoezi la upimaji wa Corona Virus kwa Wabunge wote na zoezi linatarajiwa kufanyika katika kliniki ya Bunge, Lusaka
Karani wa Bunge, Cecilia Mbewe amesema hadi kufikia Julai 15, Wabunge 3 wamekutwa na COVID19, pia wafanyakazi 10 wa Bunge wamekutwa na maambukizi pamoja na wengine 6 ambao sio wafanyakazi wa Bungeni

No comments:
Post a Comment