Rais Trump amesaini sheria kuwawekea maafisa wa China vikwazo kuhusiana na matendo yao ya ukandamizaji dhidi ya Wahong Kong. Trump pia amesaini amri ya kumaliza uhusiano wa Marekani unaoipendelea Hong Kong.
Sheria aliyosaini Trump pamoja na amri ya rais, ni sehemu ya mashambulizi ya utawala wa Trump, dhidi ya China kuhusu kile anachosema ni matendo yasiyo sawa ya taifa hilo la Asia.
Shutuma hizo za karibu kila siku, za Trump dhidi ya China, zimejiri mnamo wakati Trump akijitetea dhidi ya ukosoaji kuhusu anavyolishughulikia janga la corona huku kukiwa na ongezeko la maambukizi mapya nchini mwake.
"Sheria hii inaupa utawala wangu zana mpya zenye nguvu kuwawajibisha watu na taasisi ambazo zimehusika kuipokonya Hong Kong uhuru wake. Sote tumeona kile kilichofanyika. Si hali nzuri. Uhuru wao umechukuliwa, haki zao zimechukuliwa, na kwa maoni yangu kutokana na hayo Hong Kong haipo kwa sababu, haitaweza tena kushindana na masoko huru.” Amesema Trump.
China tayari imesema italipiza kisasi dhidi ya hatua hiyo ya Trump, itakayoruhusu pia mabenki kuwekewa vikwazo kuhusiana na hatua yake dhidi ya Hong Kong.
Kwenye taarifa, wizara ya Mambo ya nchi za nje ya China imesema kipengee cha sheria ya Hong Kong kuhusu utawala wa ndani kinaikosea heshima sheria ya taifa kuhusu usalama, ambayo China iliuwekea mji huo hivi karibuni.
Wizara hiyo imeongeza kwamba China itatoa majibu yanayostahiki ili kuyalinda masilahi ambayo ni halali, na pia itaweka vikwazo kwa maafisa wa Marekani na kampuni zake.
Muswada ambao Rais Trump amesaini kuwa sheria unavilenga vikosi vya polisi ambavyo vimewakandamiza waandamanaji wa Hong Kong, pamoja na maafisa wa Chama cha Kikomunisti kinachotawala China wanaohusishwa na sheria ya taifa ya usalama wa China kwa Hong Kong, inayotizamwa kupunguza nguvu ya utawala wa ndani wa Hong Kong.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Sekta ya Ujenzi, Arch. Elius Mwakalinga, akitoa maelekezo kwa Kai...

No comments:
Post a Comment