Madarasa 11 kati ya 15 ya Shule ya Sekondari ya Kinondoni Muslim iliyoko Kinondoni Shamba Jijini DSM yameteketea kwa moto.
Mbali ya majengo hayo vifaa na samani za shule hiyo vimeteketea kwa moto huku Walimu na Wanafunzi wote wa shule hiyo wapatao 218 wakisalimika.
Maafisa wa Jeshi la Zimamoto wamesema ni muhimu maeneo yote ya shule yakawa na maji ya dharura ili kujikinga na madhara ya moto.
Msaidizi wa Mkuu wa Shule amesema “hali ya Watoto ipo vizuri hakuna alieathirika ila vitu vyote vimeteketea, hakuna kilichobaki na madarasa yote 11 kati ya 15, masomo yataendelea tuna Shule nyingine watahamishiwa Shule nyingine ya kwetu”.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment