SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) rasmi imeruhusu kuendelea kwa Shughuli zote za Michezo pamoja na kuruhusu Mashabiki kuingia Viwanjani na kuwataka kuendelea kuchukua tahadhari ya maradhi ya Covid 19.
SMZ ilitoa katazo la kuzua shughuli mbalimbali ikiwemo michezo na kuzuia mashabiki kuingia viwanjani kutokana na mripuko wa homa kali ya mapafu (Covid 19) inayosababishwa na virusi hatari vya corona.
Ikumbukwe kwamba June 5, 2020 SMZ iliregeza masharti na kuanza kuruhusu kwa baadhi ya shughuli kurejea huku Ligi kuu soka Zanzibar pekee iliruhusiwa kutumuia vumbi katika viwanja tofauti tofauti bila ya kuwa na mashabiki.
Akitoa taarifa rasmi ya Serikali kwa vyombo vya Habari, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohammed Aboud Mohammed amesema Serikali imefikia uwamuzi huo kutokana na kupungua kwa kiasi kikubwa cha uogonjwa wa Covid 19 uliukumba Zanzibar na ulimwengu kwa ujumla.
"Kuanzia sasa shughuli zote za michezo ambazo zitahusisha ligi kwa madaraja yote yataruhusiwa kuendelea kuchezwa huku mashabiki nao wakiruhusiwa kuingia viwanjani" alisema Waziri Aboud.
Pia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, imefungua rasmi vyuo vya Qur-ani (Madrasa) na elimu zinazotolewa na taasisi nyengine za kidini zikiwemo madarasa za watu wazima misikitini, madarasa za akina mama, na shughuli zote za mikusanyiko za elimu ya kidini.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment