Search This Blog
Sunday, July 5, 2020
Hatma ya wanafunzi, shule iliyoungua Ilala
Wanafunzi watatu katika shule ya sekondari Islamic ilipo ilala Jijini Dar es Salaam wamefariki dunia kufuatia ajali mbaya ya moto ulizuka majira ya saa nane za usiku ukianzia katika mabweni wa shule hiyo.
Akizungumza na waandisha wa habari akiwa katika eneo la tukio mapema leo, Mkuu wa wilaya ya Ilala, Bi Sophia Mjema amesema moto huo ulianza kuwaka usiku na jitihada zilizofanywa zilifanikiwa kuwaokoa wanafunzi wengi lakini bahati mbaya wanafunzi watatu walikutwa wamepoteza maisha.
Mkuu huyo wa wilaya ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama amesema chanzo cha ajali hiyo hakijajulikana ingawa tayari ameunda kamati ili kubaini chanzo cha ajali hiyo.
Hata hivyo mkuu wa wilaya ameruhusu watoto kwenda kusoma kwa muda katika shule za jirani ili wasikose masomo lakini pia serikali kwa kushirikiana na uongozi wa shule kuweka mazingira mazuri ya kusomea katika kipindi hiki cha mpito.
Naye Shekh Mkuu wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum amesema anaichukulia ajali hiyo kama janga hivyo kama kiongozi wa dini anatoa pole kwa uongozi wa shule serikali na familia za watoto waliokumbwa na ajali hiyo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment