Search This Blog
Saturday, July 11, 2020
Gigy Awachefua Mashabiki...Kutema Tema Mate Ovyo Kwampoza
MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Gift Stanford ‘Gigy Money’ mapema wiki hii amewakera mashabiki zake mtandaoni baada ya kuposti video akiwa anaswaki na kutema mate hovyo, jambo lililofanya kila mmoja kuongea lake.
Mwanamama huyo asiyeishiwa vituko mjini, aliposti video hiyo na kuandika hivi “Mwenye kinyaa afe, ulitumwa? (Am savage and nasty) wee amekutuma nani?” aliandika Gigy.
Baada ya kuona hivyo, baadhi ya mashabiki zake walimjia juu na kila mtu kuongea lake ambapo kuna baadhi walisema anatakiwa ajiheshimu kwa sababu yeye ni kioo cha jamii na ni mama hivyo anapofanya vitu awe na mipaka.
“Jamani huyu dada hajiheshimu hata kidogo, sasa ndiyo nini kuonyesha huo uchafu wake hapa? Ndiyo maana Mo J alimuacha hata ningekuwa mimi nisingeweza kuvumilia ujiga huu, yaani anatia kinyaa,” alikomenti shabiki mmoja aliyefahamika kwa jina la @Maggie.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment