Search This Blog
Tuesday, June 16, 2020
Watanzania 249 waliokwama nchini India warejea nyumbani
Zaidi ya abiria 249 wamewasili hapa nchini baada ya kukwama nchini India kwa zaidi ya miezi mitatu kufuatia mlipuko wa virusi vya corona ulioikumba dunia na kusababisha nchi nyingi kufunga safari za kutoka na kuingia katika nchini hizo.
Wakizungumza na Channel Ten katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam baadhi ya abiria waliorejea nchini pamoja na ndugu waliokuja kuwalaki wameipongeza na kuishukuru serikali ya Tanzania kwa hatua iliyochukua kuwaandalia ndege kwa ajili ya safari ya kurejea hapa nchini, hatua ambayo wamesema ni kielelezo cha kuwajali wananchi wake.
Naye Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Shirika la Ndege la Tanzania ATCL Josephat Kagirwa amesema kwamba shirika hilo limehakikisha safari inafanikiwa na litaendelea kutoa huduma za usafiri ipasavyo ikiwemo ya kuwarejesha abiria walio kwama katika nchi mbalimbali.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment