Search This Blog
Tuesday, June 16, 2020
Wezi wa mifugo wageuzwa kuwa kama Ng'ombe
Watu wawili wanaosadikiwa kuwa ni wezi wa mifugo katika Kijiji cha Busegwe Wilayani Butiama Mkoani Mara, wamekumbwa na hali ya kula majani kama Ng'ombe, mara baada ya wanakijiji kushirikiana na familia iliyoibiwa Ng’ombe, kumuita mganga kutoka nchini Kenya na kufanya dawa hiyo.
Imeelezwa kuwa tukio hilo la aina yake limetokea jioni ya Juni 15, 2020, ambapo lengo kuu la kumuita mganga huyo, ilikuwa ni kuwarudisha watu waliomuiba Ng'ombe mwenye thamani ya Shilingi Milioni 2 kwa kuwa tabia ya wizi wa mifugo kijijini hapo, imekithiri kwa kiasi kikubwa.
Imeelezwa kuwa mara baada ya dawa hiyo kufanyika, watu hao walirudi na kuanza kukata majani na kuyala kama wafanyavyo Ng'ombe, kitendo ambacho wamekifanya wakiwa kwenye hali ya kutojitambua, huku wakishuhuduwa na wana Kijiji.
Kwa upande wake mmiliki wa Ng'ombe aliyeibiwa Grace Jonathan, ameeleza ni kwa namna gani alibaini kama mfugo wake hayupo zizini, "Ng'ombe huyo aliibiwa usiku wa kuamkia ijumaa(Wiki iliyopita), mwanzo hatukugundua lakini, watoto wakati wanaenda kuchunga ndiyo tukabaini kwamba Ng'ombe hayupo, tukaja kuangalia Zizi la Ng'ombe limekatwa, moja kwa moja tukajua kaibiwa kwahiyo msaada mbadala ndiyo tulioutumia, na ndiyo hiki mnachokiona hapa".
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment