Search This Blog

Thursday, June 18, 2020

Mjumbe kamati kuu CHADEMA ajivua vyeo na kujiunga CCM


Ndugu Moses Matiko Misiwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Tarime Vijijini, Mkoa wa Mara na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema leo amejivua vyeo vyake vyote ndani ya Chama hicho na kuomba kujiunga na CCM.

Aidha Ndugu Moses Matiko Misiwa ameeleza sababu za kuachana na Chama chake,amesema chama hicho kwa sasa  kimepoteza muelekeo, Hivyo Uongozi wa dhati na wenye matokeo chanya wa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Taifa Dk. John Pombe Joseph Magufuli na Uimara wa CCM kwa sasa katika kuwatumikia Watanzania ndio umemkuna zaidi na hatimaye kuchukua uamuzi alioufanya.

Ndugu Matiko amepokelewa na Ndugu Humphrey Polepole na kumhakikishia kuwa amefanya chaguo sahihi kwa wakati sahihi.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...