Search This Blog
Thursday, June 18, 2020
Bolton amshutumu Trump kwa kutafuta msaada wa China ili aweza kuchaguliwa tena
Mshauri wa zamani wa rais wa Marekani Donald Trump kuhusu usalama wa kitaifa, John Bolton amemshutumu rais Trump kwa kutafuta msaada kutoka China ili aweze kushinda uchaguzi wa urais uliopangwa kufanyika mwezi Novemba mwaka huu.
Kulingana na kitabu John Bolton alichoandika na ambacho ikulu ya Marekani imeshitaki kutaka kisizinduliwe, rais Donadl Trump alimtaka kiongozi wa China Xi Jinping kumsaidia ili achaguliwe tena katika muhula wa pili kwenye uchaguzi mkuu ujao mwaka huu.
John Bolton amesema kwamba mwezi Juni 2019, Donald Trump "aligeuza mazungumzo kuhusu uchaguzi ujao wa urais, kwa kuzingatia uwezo wa kiuchumi wa China na kwa kumrai rais wa China Xi Jinping kumsaidia ili aweze kushinda katika uchaguzi huo”, kulingana na baadhi ya maneneo yaliyochapishwa na Magazeti ya Wall Street, New York Times na Washington Post.
Wakati wa mkutano huu kando ya mkutano wa kilele wa G20 huko Osaka, rais wa Marekani "alisisitiza umuhimu wa wakulima na kuongezeka kwa ununuzi wa bidhaa kutoka China hususan soya na ngano ikiwa atachaguliwa tena kwa muhula wa pili kuwa rais wa Marekani", ameandika kwenye kitabu chake.
Bolton amedai kuwa nia ya Trump kutaka kuchaguliwa tena ndiyo imekuwa msingi wa sera yake ya mambo ya kigeni.
Kitabu hicho kinachoitwa “The Room Where it Happened” yaani Chumba ambacho kilitokea’ kinatarajiwa kuzinduliwa Jumanne ya wiki ijayo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment