Search This Blog
Monday, June 15, 2020
Donald Ngoma atemwa rasmi Azam FC
UONGOZI wa Azam FC umethibiisha kuachana rasmi na nyota wa zamani wa Yanga, Donald Ngoma, baada ya mkataba wake kufikia ukingoni Juni 14.
Ngoma alijiunga na Azam FC akitokea Klabu ya Yanga ambapo aliweza kutwaa Kombe la Mapinduzi mwaka jana na Kombe la Shirikisho la Azam Sports (ASFC) msimu uliopita.
Kwa kipindi chote cha misimu miwili, alichodumu ndani ya Azam FC, Ngoma amekuwa mmoja ya washambuliaji wa kutumainiwa akiwa mfungaji bora wa timu yetu msimu uliopita kwa mabao yake 14 aliyoifunga kwenye mashindano yote.
Hadi anamaliza mkataba wake kwenye timu hiyo yenye maskani yake Azam Complex, Chamazi, Ngoma amefanikiwa kucheza jumla ya mechi 42 za mashindano yote, akihusika katika mabao 20, baada ya kufunga 16 na kutoa pasi za mwisho nne.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment