Search This Blog
Thursday, June 11, 2020
Anayetajwa kutua Young Africans awaaga Rayon Sports
Hatimaye kiungo anayehusishwa kujiunga na Young Africans, Fabrice Mugheni, amewaaga rasmi mashabiki wa timu yake ya Rayon Sports ya Rwanda kwa kuwaambia ataondoka mwishoni mwa msimu huu.
Fabrice raia wa DR Congo aliwahi kusema kuwa, aliombwa video zake na Injinia Hersi Said ambaye ni Mkurugenzi wa Uwekezaji GSM ambaye pia anahusika na masuala ya usajili ndani ya Young Africans.
Fabrice kupitia mtandao wake wa Instagram, aliwaaga rasmi mashabiki wa timu hiyo jambo ambalo linatafsiriwa kama huenda akawa alishamalizana na Young Africans kwa ajili ya kujiunga na timu hiyo.
Young Africans wamekua wanahusishwa na mipango ya usajili wa baadhi ya wachezaji wa kimataifa, hii ni kwa ajili ya kujipanga vyema kwa msimu ujao wa Ligi Kuu na michuano ya kimataifa, endapo watapata fursa ya kuiwakilisha nchi kupitia michuano ya Kombe La Shirikisho.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment