Wakati ndoto ya Taifa ikiwa imejikita katika kutekeleza sera ya uchumi wa viwanda ifikapo mwaka 2025, Wilaya ya Magu mkoani Mwanza inatarajia kujenga kiwanda cha kutengeneza vipodozi vitokanavyo na zao la Parachichi, ili kuunga mkono sera hiyo ya awamu ya tano.
Kampuni ya uwekezaji ya Nkonya Farms Ltd itakayojenga kiwanda hicho, imekwishapanda zaidi ya miche 2,000 ya parachichi huku ikitangaza soko kwa wakulima wa zao hilo wilayani Magu, kuchangamkia fursa ya kilimo hicho.

No comments:
Post a Comment