Search This Blog
Thursday, May 21, 2020
Lukaku sitamsamehe kamwe Andre Villas-Boas
Mshambuliaji wa Inter Milan ya Italia Romelu Lukaku ameeleza hasira zake kwa kocha wa zamani wa Chelsea Andre Villas Boas kuwa hawezi kumsamehe kwa sababu ya kumuacha katika kikosi cha UEFA Champions League 2011/12.
“Kocha (Roberto) Di Matteo aliniambia kuwa nitakuwa pamoja na timu hadi baada ya fainali, alifikiria kuwa kila mmoja anatakiwa kuja kusherehekea (Ubingwa) waliokuwa wamesimamishwa na hata ambao hawakuwa kwenye kikosi cha Champions League, namshukuru kwa hilo (Di Matteo)”-Lukaku
“Hili taji (UCL) ni moja kati ya mataji niliyokuwa nayaota, unatakiwa usherehekee Ubingwa ule ukiwa kwenye timu lakini kuna mtu mmoja ambaye alinitoa (Kikosini) kocha aliyepita (Andre Villas-Boas) sitamsamehe kamwe katika sherehe zile sikushika lile Kombe kwa vidole vyangu sababu sikuwa nimeshiriki kulitwaa”-Lukaku
Lukaku aliwasili Chelsea 2011 kwa uhamisho wa pound milioni 17 lakini hakupata nafasi chini ya kocha Andre Villas-Boas na hakumjumuisha katika kikosi cha Champions League, baadae Boas alifukuzwa na nafasi yake kurithiwa na Di Matteo ambaye alitwaa Ubingwa na kuamua kumchukua Lukaku katika sherehe za Ubingwa waliporejea London wakitokea Munich ilikopigwa fainali.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment