Search This Blog
Sunday, May 3, 2020
Kipa wa Yanga akwama nchini Kenya
FAROUK Shikalo, kipa namba moja wa Yanga amekwama nchini Kenya ambako alikwenda kwa ajili ya mapumziko yaliyotolewa na Serikali kutokana na maambukizi ya Virusi vya Corona.
Ofisa Habari wa Yanga, Hassan Bumbuli amesema kuwa wachezaji wote wa kigeni kwa sasa wapo Bongo isipokuwa Shikalo ambaye yupo Kenya.
"Wachezaji wote wakigeni wapo hapa Bongo kwa sasa isipokuwa Shikalo ambaye yupo Kenya alikokwenda kwa ajili ya mapumziko ila kwa sasa mipaka imefungwa kutokana na maambukizi ya Virusi vya Corona," .
Ligi Kuu Tanzania Bara ilisimamishwa Machi 17 kutokana na maambukizi ya Virusi vya Corona ambavyo vimekuwa ni janga la dunia kwa sasa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment