Kimbunga kikubwa ambacho hakijatokea miongo kadhaa iliyopita cha Amphan, kimeipiga India upande wa mashariki leo jumatano, kikiwa na upepo unaotembea hadi kilometa 190 kwa saa.
Mkurugenzi wa hali ya hewa nchini India Sanjib Banerjee amesema kimbuga hicho kimeipiga kisiwa cha Sagar kilichopo katika pwani ya India.
Afisa huyo wa hali ya hewa amesema kimbunga kinaweza kusababisha madhara zaidi India na Bangladesh, ambapo wakazi milioni kadhaa katika eneo la Pwani wameondolewa kukimbia kimbunga hicho.
No comments:
Post a Comment