Search This Blog
Wednesday, May 20, 2020
Hizbullah: Tumejiandaa barabara kuzima uchokozi wowote wa Israel
Afisa mwandamizi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon amesema harakati hiyo ya muqawama imejiandaa vilivyo na ipo tayari kikamilifu kukabiliana na uvamizi na chokochoko zozote za utawala wa Kizayuni wa Israel.
Sayyid Hashem Safieddine, Mkuu wa Baraza Kuu la Utendaji la Hizbullah amesema hayo katika mahojiano na kanali ya televisheni ya al-Mayadeen ya Lebanon na kueleza bayana kuwa, "harakati ya muqawama imejiandaa vilivyo na tumekwishaainisha machaguo ya kuchukua iwapo tutajikuta katika makabiliano na maadui."
Hata hivyo amesisitiza kuwa, harakati hiyo ya Kiislamu haifuatilii vita na wala haitaki kuchochea vita, lakini imejiandaa barabara kuzima uchokozi wowote wa maadui.
Kadhalika Sayyid Hashem Safieddine ameashiria kuhusu kadhia ya Palestina na kubainisha kuwa, "ukombozi wa Quds Tukufu toka mikononi mwa Wazayuni maghasibu ni katika ajenda kuu za harakati za muqawama katika eneo."
Aidha Mkuu wa Baraza Kuu la Utendaji la Hizbullah ya Lebanon amekumbusha kuwa, jeshi la Israel litaendelea kushindwa na kukabiliwa na vipigo kama lilivyoshindwa na harakati za muqawama miaka ya nyuma katika eneo hili la Asia Magharibi, vikiwemo vipigo vikali lilivyopokea katika vita lilivyoanzisha mwaka 2000 na 2006 dhidi ya Lebanon.
Hali kadhalika amesisitizia umuhimu wa kuadhimishwa na kubakia katika nyoyo za ulimwengu wa Kiislamu Siku ya Kimataifa ya Quds, ambayo huadhimishwa kote duniani Ijumaa ya mwisho ya mwezi mtukufu wa Ramadhani kila mwaka.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment