Search This Blog

Tuesday, April 14, 2020

Umoja wa Ulaya kutoa msaada wa Euro milioni 80 Sudani kwa ajili ya kupambana na virusi vya Corona


Umoja wa Ulaya katika juhudi za kupambana na virusi vya corona  umefahamisha kwamba utatoa msaada wa Euro milioni 80 kwa Sudani kwa ajili ya kuzuia na kupambana na maambukizi ya virusi vya corona.

Msaada huo utatolewa kwa lengo la kuhakikisha kwamba  idara ya afya nchini humo haisumbuki katika juhudi zake dhidi ya virusi vya corona.

Jarida rasmi la Sudani limefahamishakuwa Abdullah Hamduk amezungumza kwa njia ya simu na  kamishana wa masuala  ya ushirikiano wa kimataifa  Umoja wa Ulaya Jutta Urpilainen.

Imefahamishwa kuwa katika mazungumzo yao hao, kamishna huyo wa Ulaya amesema kuwa Umoja wa Ulaya utatoa kiwango cha Euro milioni 80 kwa Sudani kwa ajili ya kukabiliana na virusi vya corona.

Waziri wa afya wa Sudani  Ekrem ali et Tum alifahamisha kuwa wizara yake inahitaji kiwango cha  dola milioni 120  ili kukabiliana na virusi vya corona.

Watu wanne wamekwishafariki kwa virusi vya corona nchini Sudani hum-ku watu wengine 29 wakiripotiwa kuwa na maambukizi ya virusi hivyo.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...