Rais Donald Trump wa Marekani amesema mataifa yanayozalisha mafuta kwa wingi duniani (OPEC) pamoja na wazalishaji wengine wana mpango wa kupunguza uzalishaji wa mapipa milioni 20 kwa siku, ikiwa ni mara mbili ya mapipa milioni 10 ambayo yaliridhiwa siku moja kabla.
Katika taarifa yake ya Twitter, Trump amesisitiza sio mapipa milioni 10 kama ilivyoripotiwa katika maeneo mengi.
Mataifa hayo ya OPEC yakiwa ni Urusi na nchi zingine Jumapili yalisema yameridhia kupunguza uzalishaji wa mapipa milioni 9.7 kwa siku katika miezi ya Mei na Juni, baada ya siku nne za mazungumzo pamoja na shinikizo la Rais Trump la kuzitaka pande husika kufikia makubaliano juu ya kudhibiti bei ya petroli iliyoshuka zaidi.

No comments:
Post a Comment