Search This Blog
Monday, April 20, 2020
Mchekeshaji PIERRE LIQUID Athibitika Kuwa na Virusi vya Corona...
Mchekeshaji Peter Mollel maarufu kama Pierre Liquid amebainika kuwa na maambukizi ya #COVID19 na sasa yupo Hospitali ya Amana akiendelea na matibabu
Amesema, "Nina bosi wangu wa karibu ambaye kapata ugonjwa huu na kwa kuwa mara nyingi tuko naye alinishauri na mimi nikapime kwa nia njema ili kama ninao nipate matibabu mapema na kuepuka kuwaambukiza wengine”
Ameongeza, "Nilienda hospitali ya Temeke, wakanipima ndipo nilipokutwa ninao na kuletwa hapa Amana ambapo kwa sasa ni moja ya kituo cha wagonjwa.”
Hata hivyo, amesema kuwa yeye anahisi atakuwa ameambukiziwa baa maana ndio maeneo yake ya kujidai na hivyo amewapongeza baadhi ya viongozi waliotoa tamko la kufungwa kwa baa akisema ni hatua nzuri
Amesisitiza kuwa maeneo ya baa watu kuwa makini kujikinga na ugonjwa huu ni ngumu na pia huusisha mikusanyiko ambapo mtu akiwa hajalewa anaweza kukaa mbali na watu lakini pombe zikishamuingia akili hiyo haitakuwepo tena
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment