Search This Blog

Wednesday, April 22, 2020

Dc Kimanta aridhishwa na ujenzi wa nyumba za walimu shule ya Ole Sokoine


Na John Walter- Monduli.

Mkuu wa Wilaya ya Monduli Iddi Kimanta  ameitembelea shule ya Sekondari Ole Sokoine  iliopo kata ya Monduli juu na kukagua hatua za ujenzi wa nyumba mbili za walimu.

Gharama  za ujenzi wa nyumba hizo inatajwa kuwa shilingi milioni  mia moja (100) huku wananchi wa Kata za Monduli juu na Mfereji ambao watoto wao wanasoma katika shule hiyo wakiunga mkono hatua hizo ya ujenzi  kwa kufanya kazi za mikono kwa  kuchimba msingi,kukusanya mawe pamoja na kuchimba mashimo ya vyoo ili  walimu waweze kuwa karibu na shule na kuwafanya wanafunzi wafanye vizuri katika masomo yao.

Aidha  Kimanta amewapongeza  wananchi hao kwa kuunga mkono jitihada hizo za mandeleo.

Katika ziara hiyo Mkuu wa wilaya Iddi Kimanta aliongozana na  Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya hiyo Stephine Ulaya na Mhandishi wa wilaya Eng. Peter Shemahonge.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...