Search This Blog

Sunday, April 19, 2020

Canada na USA zarefusha hatua ya kufunga mpaka wao

Kutokana na janga la virusi vya corona mpaka kati ya Marekani na Canada utaendelea kufungwa.

Waziri mkuu wa Canada Justin Trudeau ametangaza kuwa hatua hizo zilizofikiwa kwa pamoja kati ya Marekani kwamba zimerefushwa kwa muda wa mwezi mmoja. Mpaka huo ulikuwa umefungwa kwa zaidi ya wiki tatu.

Hata hivyo mpaka huo utaendelea kuwa wazi kwa ajili ya kupitisha bidhaa. Kabla ya kuzuka kwa janga la virusi vya corona zaidi ya watu 400,000 huvuka mpaka huo karibu kila siku.

Mpaka huo wenye urefu wa kilometa 8,900 ni mrefu zaidi duniani.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...