Search This Blog

Tuesday, March 10, 2020

Baraza jipya la mawaziri nchini Malesia laapishwa


Waziri mkuu wa Malesia, Muhyiddin Yasin atangaza baraza lake jipya la mawaziri, kisha mawaziri hao walikula kiapo na kuanza majukumu yao.

Mawaziri 31 na manaibu waziri 38 walikula kiapo katika kasri la kifalme mjini Kuala Lumpur wakishuhudiwa na mfalme wa Malesia Sultan Abdullah Shah.

Waziri mkuu Muhyiddin naye alihudhuria dhifa hiyo ya kula kiapo kwa mawaziri.

Mawaziri wa Malesia ni sharti wawe wabunge na wajumbe wa baraza la mawaziri.

Jana Muhydin akiwa katika ofisi ya waziri mkuu alitangaza baraza lake la mawaziri na kwa mara ya kwanza tofauti na ilivyoada hakutakuwa na nafasi ya waziri mkuu msaidizi.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...