Search This Blog
Monday, March 9, 2020
Aston Villa yachapwa bao 4-0 na Leicester City
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta usiku wa jana amecheza kwa dakika zote 90, timu yake, Aston Villa ikiendelea kuvurunda katika Ligi Kuu ya England baada ya kuchapwa 4-0 na wenyej, Leicester City Uwanja wa King Power.
Kipigo kinazidi kuiporomosha Aston Villa inayofundishwa na kocha Muingereza, Dean Smith sasa ikibaki na pointi zake 25 baada ya kucheza mechi 28 na kuendelea kukamata nafas ya 19, ikiizidi pointi nne Norwich City inayoshika mkia katika ligi ambayo mwisho wa msimu timu tatu zitateremka daraja.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Michael Oliver, mabao ya Leicester City inayofundishwa na kocha wa zamani wa Liverpool, Brendan Rodgers yalifungwa na Harvey Barnes dakika ya 40 na 85 na Jamie Vardy mawili pia, dakika ya 63 kwa penalti na 79.
Kwa ushindi huo, Leicester City inafikisha pointi 53 baada ya kucheza mechi 29 na kuendelea kukamata nafasi ya tatu, nyuma ya Manchester City yenye pointi 57 za mechi 28 na Liverpool yenye pointi 82 za mechi 29.
Kikosi cha Leicester City kilikuwa; Schmeichel, Pereira, Evans, Soyuncu, Justin, Ndidi/Mendy dk84, Albrighton, Praet/Tielemans, Maddison, Barnes na Iheanacho/Vardy dk60.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment