Search This Blog

Saturday, February 29, 2020

WHO: Maswali Ambayo Kila Waziri wa Afya Anapaswa Kujiuliza Kuangalia Utayari wa Kupambana na Corona



Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Dkt. Tedros Ghebreyesus ametoa maswali ambayo kila Waziri wa Afya inabidi ajiulize kujua utayari wa nchi kupambana na #Corona. Baadhi ya maswali hayo ni...

Je, tutafanya nini iwapo tunapata mgonjwa wa #corona?. Je, tuna kitengo cha karantini kwa wagonjwa?. Je, tuna Oksijeni ya kutosha na vifaa muhimu?

Je, wahudumu wetu wa afya wana mafunzo na vifaa ili wawe salama?. Je, wahudumu wa afya wanafahamu jinsi ya kufanya uchunguzi kutoka kwa wagonjwa?

HIZI HABARI KAMA HIZI ZINAPATIKANA KWENYE APP YA UDAKU SPECIAL DOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL BLOG <DOWNLOAD HAPA>

Je, katika viwanja vya ndege na mipakani tuna mikakati ya kuchunguza watu iwapo ni wagonjwa?. Je, maabara zetu zina vitendea kazi vya kuchunguza sampuli?

Je, Hospitali zetu na Kliniki zina kanuni sahihi za kukinga na kuzuia maambukizi?. Je, Wananchi wana taarifa sahihi?. Je, wanafahamu dalili za ugonjwa husika?

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...