Search This Blog
Saturday, February 29, 2020
Acha Tabia Hizi..Haziendani na Utanashati.....
Mdau wa JamiiForums ameelezea baadhi ya tabia ambazo mtu akizifanya mbele ya Umma zinaondoa utanashati wake na kumshusha hadhi kabisa. Ameshauri Watu kuacha tabia hizo
Mdau amewashauri watu kuacha kutoa uchafu puani kwa vidole vyao maana pua ina bakteria wengi sana na badala yake watumie kitambaa. Pia, ameshauri kuacha kujishika sehemu za siri ndani ya nguo hata kama zinawasha na ikitokea unawashwa jikunie kwa nje ya nguo
Ameshauri pia kuacha kupenga kamasi kwa mikono mitupu na badala yake hakikisha unakuwa na kitambaa maalumu. Lakini pia ameshauri kunika nguo zako za ndani kwenye jua la kutosha na pia nawa maji ukitoka chooni kwa haja ndogo au kubwa
Amedai kuwa Muungwana yeyote anakuwa na kitambaa cha kujifutia jasho ukijiona unatembea bila ya kitambaa wewe ni mchafu. Mwisho ameshauri kuwa hakikisha makalio yako unayapaka mafuta, hasa wanaume ambao kwa asilimia kubwa hawapaki mafuta
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment