Mamlaka ya Mawasiliano nchini Tanzania (TCRA) imetoa wito kwa Watanzania waliokamilisha usajili wa laini zao kuhakiki upya.
Katika taarifa iliyotolewa leo Alhamisi, mkurugenzi mkuu wa TCRA, James Kilaba amesema mchakato huo unapaswa kufanyika kabla ya simu ambazo hazijasajiliwa kuzimwa Januari 20, 2020.
Kumekuwa na hofu kuwa mamilioni ya watu wanaomiliki simu za mkononi nchini Tanzania huenda wakakosa mawasiliano ya simu kutokana na kufungwa kwa laini zao za simu ambazo hazijasajiliwa kwa alama za vidole.
Mwananchi mmoja mjini Dodoma Haruna Mkupe anasema ''Nimefuatilia namba yangu kwa NIDA tangu mwezi wa tano mpaka sasa sijapata namba yangu, tunapata taabu kwa sababu pia ya umbali wa ofisi za NIDA''
Doris anasema amechelewa kujiandikisha kwa sababu ya pilika nyingi za maisha: ''Nilichukua fomu nimejaza nimekuja kukamilisha usajili wa NIDA, nilikuwa nikiishi nje ya mkoa wa Dodoma, dakika za majeruhi hizi.''


No comments:
Post a Comment