Aliyekuwa Kaimu Kocha Mkuu wa Yanga, Boniface Mkwasa, amesema kuwa hajui hatima yake ndani ya klabu hiyo mara baada ya ujio wa kocha mpya Mbelgiji, Luc Eymael.
Yanga imemleta Eymael kuchukua nafasi ya Mwinyi Zahera ambapo Mkwasa alikuwa akikaimu kwa muda tangu kutimuliwa kwa Zahera mwishoni mwa mwaka jana.
Mkwasa amesema kuwa, kwa sasa bado hajui hatima yake ndani ya kikosi hicho baada ya kocha mpya licha ya kuendelea kuwepo kikosini, huku akisema hafahamu kama atabaki au la.
“Tumefurahi ujio wa kocha mpya ndani ya Yanga na tutatoa ushirikiano wa kutosha kuhakikisha anafanya kazi vizuri kwa kumuelekeza utaratibu wote wa timu.
“Kwa upande wangu bado sijajua hatma yangu viongozi ndiyo wanaojua na ndiyo wenye majibu kuhusu uwepo wangu ndani ya timu, kwa sasa bado naendelea kukinoa kikosi hadi kocha mpya atakapotambulishwa rasmi kwani kwa sasa bado hajakabidhiwa kikosi,” alisema Mkwasa
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment