Search This Blog

Thursday, January 16, 2020

Maxime awaita Yanga mezani

By Saddam Sadick

Mwanza. Kocha wa Kagera Sugar Mecky Maxime amesema yuko tayari kujiunga na Yanga endapo klabu hiyo itampa dau analotaka.

Kauli ya Maxime imekuja muda mfupi baada ya kuiongoza Kagera kupata ushindi wa mabao 3-0 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, juzi.

Akizungumza jana, Maxime alisema ingawa ana sifa ya kuwa kocha mkuu, lakini kama Yanga wanamtaka atakuwa tayari kuwa msaidizi wa Luc Eymael.

Maxime aliyewahi kuinoa Mtibwa Sugar, alisema amefungua milango kwa Yanga kama wameridhishwa na kazi yake.

“Nina Leseni A ya Caf (Shirikisho la Soka Afrika), Yanga wananihitaji niwe kocha msaidizi sina tatizo mimi naangalia maslahi wakinipa zaidi ya ninachopata Kagera Sugar nitaenda” alisema kocha huyo.

Kocha huyo alisema anaendelea kuheshimu mkataba wake na Kagera na klabu inayomtaka inapaswa kufuata utaratibu.

Advertisement

Pia Maxime aliwapongeza wachezaji kwa kazi nzuri waliyofanya katika mchezo dhidi ya Yanga kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Let's block ads! (Why?)

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...