Search This Blog

Thursday, December 26, 2019

Waziri Mkuu wa Sudan kuwafikisha Mahakamani wahalifu wa mauaji ya kimbari


Waziri Mkuu wa Sudan Bw. Abdalla Hamdok aahidi kuwafikisha mahakamani wanaohusika na mauaji ya kimbari.

Bw. Hamdok amesema hayo akitoa hotuba katika mkutano wa kuadhimisha mwaka mmoja wa maandamano ya Desemba ya Sudan, huku akisema haki itatendeka, sheria itafuata mkondo dhidi ya wauaji wote.

Ameongeza kuwa uhalifu wa kivita na mauaji ya kimbari hauna ukomo wa muda wa kisheria, juhudi zitafanyika kuhakisha wahalifu wote wanafikishwa mahakamani na heshima kwa familia za wafiwa inarejeshwa.

Watu wa Sudan wanasherehekea maadhimisho ya mwaka mmoja tangu maandamano yafanyike Desemba 19 mwaka jana. Kutokana na shinikizo mitaani, jeshi la Sudan Aprili 11 lilimwondoa madarakani rais wa zamani Omar al-Bashir na kuunda baraza la kijeshi kusimamia mambo ya nchi.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...