Search This Blog
Sunday, December 8, 2019
Washikiliwa na Polisi wakituhumiwa kushiriki mauaji kisa ushirikina
Polisi Mkoani Mbeya wanawashikilia Watu watatu kwa tuhuma za mauaji ya John Mwakarundwa(62) Mkazi wa Kijiji cha Nkunga, Rungwe tukio ambalo linahusishwa na imani za kishirikina.
Kamanda wa Polisi Mbeya Ulrich Matei amesema Watuhumiwa walimvamia Mwakarundwa na kumkatakata na vitu vyenye ncha kali maeneo ya kisogoni, taya la kushoto na tumboni hadi kufariki.
RPC Matei amesema historia inaonesha Mwakarunda alikuwa anatuhumiwa kwenda kununua uchawi Malawi hivyo Wananchi wa eneo hilo walikuwa na hasira nae wakidai anawatesa Kijijini hapo.
"Watuhumiwa wanadai wamefanya hivyo ili kulipiza kisasi na baada ya kuuawa kwake Wananchi walikuwa wanashangilia wakifurahia kifo chake, Serikali haiwezi kujiingiza kwenye mambo hayo tutawahoji na kuwafikisha Mahakamani" amesema.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment