Search This Blog
Saturday, December 28, 2019
Upadate: Waliofariki katika ajali ya ndege Kazakhstan wafikia 15
Mamlaka ya usafiri wa anga nchini Kazakhastan imesema, idadi ya watu waliofariki katika ajali ya kuanguka kwa ndege imefikia 15.
Ndege hiyo aina ya Fokker mali ya kampuni ya ndege ya Bek iliyokuwa ikitokea Alma-ata kuelekea Nursultan ikiwa na abiria 100, ilianguka karibu na Alma-ata.
Ndege hiyo ilipotea katika rada majira ya saa 2 na dakika 5 baada ya kuondoka, baadaye ilithibitishwa kuanguka na kugonga jengo moja, lakini haikuwaka moto.
Waziri mkuu wa Kazakhastan Askar Uzakbaiuly Mamin ameiagiza idara maalumu kufanya uchunguzi kuhusu ajali hiyo, pia amesimamisha safari zote za ndege za kampuni ya ndege ya Bek nchini Kazakhastan.
Rais wa nchi hiyo Kassym-Jomart Tokayev pamoja na mtangulizi wake Nursultan Äbishuly Nazarbayev wametuma salamu za rambirambi kufuatia ajali hiyo na wameahidi kutoa misaada ya kuhitaji kwa jamaa ya watu waliofariki.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment