Search This Blog
Thursday, December 5, 2019
TAKUKURU, Skauti kutoa elimu ya rushwa Shuleni
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako, amekitaka Chama cha Skauti Tanzania kuanzisha miradi ya kilimo cha mboga mboga kwa lengo la kuinua kipato na kuwawezesha vijana wa chama hicho kuwa na uelewa wa kufanya kazi.
Akizungumza jijini Dar es Salaam Desemba 4, 2019, wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa chama hicho amesema uanzishwaji wa mradi huo utawajengea vijana hao utamaduni wa kufanya kazi kwa bidii.
Prof. Ndalichako amesema uongozi wa chama hicho ukiwa na ubunifu na nia thabiti ya kukabiliana na changamoto hakika vijana watajifunza mambo mengi mazuri na namna ya kujenga taifa lao kwa ari moja.
"Niwapongeze kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kuwafundisha vijana hao na kuwapatia elimu ambayo inawafanya watambue mambo ambayo hayafai katika taifa hili likiwamo suala la rushwa," amesema Prof. Ndalichako.
Aidha amewataka wazazi na walezi kuwaruhusu watoto wao kujiunga na chama hicho kwani kimekuwa kikiwafundisha vijana maadili mema na kupinga rushwa.
Awali Mkuu wa Skauti Tanzania, Mwantumi Mahiza, amesema kuwa ili kutatua tatizo la rushwa nchini hasa kwa kuwaandaa vijana tayari wameingia makubaliano na Taasisi ya kuthibiti na kupamba na Rushwa Tanzania (TAKUKURU), kutoa elimu kupitia skauti katika shule za msingi na sekondari nchini.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment