Search This Blog
Tuesday, December 10, 2019
Tafiti zinazofanyika nchini zatakiwa kujibu changamoto za Watanzania
Naibu Waziri Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. William Ole Nasha amesema tafiti zinazofanyika nchini zinatakiwa kujibu changamoto zinazoikabili jamii ya watanzania na Afrika kwa ujumla.
Naibu Waziri Ole Nasha ameyasema hayo Jijini Arusha akifungua Mkutano wa kumi wa Kimataifa wa Jumuiya ya Watafiti katika Malighafi Afrika (AMRS- 2019) kwa niaba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Samia Suluhu Hassan.
Kiongozi huyo amesema Tanzania imejikita katika ujenzi wa uchumi wa kati kupitia viwanda hivyo ni lazima tafiti zinazofanyika zijikite kwenye maeneo ya sayansi, teknolojia na ubunifu ili zitumike kuimarisha utengenezaji bidhaa na huduma zinazoendana na azma hiyo.
“Ni nani anaamua nini kifanyiwe tafiti, je tafiti hizo ni za kuwafaidisha waliopo nje ya nchi au watanzania? ni lazima tujikite kwenye tafiti zitakazosaidia kutatua changamoto zilizopo katika mataifa yetu na hivyo sisi wenyewe tuwe waanzilishi wa ajenda ya utafiti kulingana na mahitaji,” alisema Naibu Wazirii Ole Nasha
Kwa upande wake Rais wa Jumuiya ya Watafiti katika Malighafi ambae pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela, Prof. Hulda Swai amesema mkutano huo pamoja na mambo mengine utaainisha na kujadili maeneo ya vipaumbele vya tafiti ambavyo vitatumiwa na Vyuo Vikuu pamoja na Taasisi za kitafiti.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment