Search This Blog
Tuesday, December 10, 2019
Kundi la Al Shabaab lavamia Hoteli ya kifahari na kuua watu 10 Mogadishu
Wanamgambo wa Alshaabab nchini Somalia wamekiri kuhusika na shambulio lilotokea katika hoteli ya kifahari mjini Mogadishu SYL nchini humo. Taarifa zinasema kuwa makundi ya wanajeshi wanaonekana kwenye barabara inayoelekea katika kasri ya Rais.
Kituo cha redio cha Dalsalam mjini Mogadishu kimesema kupitia ukurasa wake wa twitter kuwa wabunge wawili kwa jina Mahgan pamoja na waziri wa zamani wa mambo ya ndani wa Somalia Abdulkadir Ali Omar wamejeruhiwa katika shambulio lilitokea katika hoteli ya SYL.
Msemaji wa Serikali, Ismail Mukhtar kupitia ukurasa wake wa Twitter amesema, Watu 10 wameuawa katika shambulio hilo ambapo Wanamgambo wa Al Shabaab watano waliovamia hoteli hiyo wameuawa na Watu wengine watano wakiwemo raia wa kawaida wawili.
Aidha, Watu takriban 82 wameokolewa na wengine wengi wamejeruhiwa huku Polisi ikitahadharisha kuwa idadi ya vifo inaweza kuongezeka kutokana na shambulio hilo katika hoteli hiyo iliyopo karibu na makazi ya Rais na inayotumiwa zaidi na Viongozi Waandamizi wa Serikali.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment