Search This Blog

Tuesday, December 10, 2019

Simba SC Yasalimu AMRI Yamrejesha Kocha Seleman Matola



Simba SC leo imetangaza rasmi kuwa kocha Seleman Matola amerejea katika timu hiyo na kujiunga nao kama kocha msaidizi akitokea club ya Polisi Tanzania aliyokuwa anaitumikia tena kama kocha msaidizi pia.

Matola anajiunga na Simba SC kwa mara nyingine baada ya miaka kadhaa kupita ambapo alikuwa kocha msaidizi Simba SC chini ya kocha wa zamani wa Simba SC Dylan Kerr, Simba SC imeahidi kuwa itatangaza kocha mkuu wa timu hiyo wiki ijayo baada ya kuachana na Patrick Aussems.
“Najisikia furaha kwa sababu nimekuwa mchezaji wa zamani wa Simba SC lakini nilikuwa kocha msaidizi wa Polisi Tanzania sasa naweza kurudi nyumbani kubwa ni kuja kushirikiana na benchi la ufundi kuhakikisha tunaisogeza Simba SC kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine”>>>Matola


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...