Rais wa Ufaransa Emanuel Macron jana ameahidi kuongeza mapambano dhidi ya makundi ya itikadi kali magharibi ya Afrika wakati vikosi vya nchi yake vikitangaza kuwauwa wanamgambo 33 wa itakadi kali nchini Mali.
Akizungumza kwenye mkutano na waandishi habari mjini Abidjan, nchini Ivory Coast, Macron amesema ni lazima kuendelea kuungana na kutia nia ya kukabili kitisho cha Itikadi kali kwenye kanda hiyo.
Jumamosi ilikuwa siku ya pili ya ziara ya siku tatu ya Macron kwenye mataifa ya Ivory Coast na Niger ambayo imetawaliwa na kuongezeka kitisho cha makundi ya itakadi kali katika eneo la Afrika Magharibi.
Katika hatua nyingine, rais wa Ivory Coast Allassane Outtara aliyekuwa mwenyeji wa Macron mjini Abdijan, ametanganza mageuzi makubwa ya sarafu ya CFA inayotumiwa na mataifa nane ya magharibi na kati ya Afrika.
Mageuzi hayo yanajumuisha kuondolewa maafisa wote wa Ufaransa kutoka vyombo vinavyosimamia sarafu hiyo pamoja na sharti la kuwekwa nusu ya akiba ya fedha za kigeni za nchi wanachama nchini Ufaransa.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment