Search This Blog
Tuesday, December 3, 2019
Ahukumiwa Jela miaka 30 kwa kosa la kumbaka Bibi wa miaka 60
Mkazi wa Kijiji cha Nange Mkoani Mwanza, Shabo Marando mwenye umri wa miaka 47 amehukumiwa kwenda jela miaka 30 kwa kosa la kumbaka Bibi wa miaka 60.
Hukumu hiyo imetolewa mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Misungwi Mkoani Mwanza Esther Malick baada ya kupitia ushahidi wa upande wa mashtaka uliokuwa na Mashahidi wanne.
Shahidi wa tatu Dkt Judith Kiwango wa Hospitali ya Wilaya hiyo amesema baada ya kumfanyia uchunguzi Bibi alimkuta na michubuko sehemu za siri na manii, Shahidi wa Pili Sama Luheka amesema alisikia kelele kichakani aliposogea alimkuta Mtuhumiwa akimbaka Bibi.
Bibi huyo ameiambia Mahakama kuwa siku ya tukio Mtuhumiwa alimkuta shambani akikusanya kuni akamkamata kwa nguvu na kumvutia kichakani kisha kumbaka.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment