Search This Blog

Tuesday, December 3, 2019

Azam FC na Mtibwa Sugar kumuenzi Jeba


Shirikisho la mchezo wa mpira wa miguu visiwani Zanzibar limeandaa mchezo wa hisani kati ya Azam FC dhidi ya Mtibwa Sugar kama sehemu ya kumuenzi kiungo za zamani wa timu hizo Ibrahim Jeba aliyefariki dunia mwaka huu.

Mchezo huo wa hisani unaolenga kukusanya pesa na kuchangia familia ya mchezaji huyo, utapigwa Desemba 9 2019 katika uwanja wa Amaan visiwani Zanzibar.

Siku ya mchezo huo zitauzwa jezi za Azam FC na Mtibwa Sugar zilizoandikwa jina la mchezaji huyo.

Jeba enzi za uhai wake aliwahi kuzichezea timu hizo mbili kwa nyakati mbili tofauti. Alifariki Dunia Septemba 19 2019 katika hospitali ya Mnazi Mmoja Unguja Zanzibar na kuzikwa Septemba 20.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...