Search This Blog
Monday, November 25, 2019
Benki ya Dunia yatoa Dola Milioni 75 kutekeleza Mradi utaoleta mapinduzi katika Elimu ya Ufundi
Serikali ya Tanzania inatekeleza Mradi unaolenga kuleta mapinduzi katika Elimu ya Ufundi Afrika Mashariki (EASTRIP) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia.
Akizungumzia mradi huo wakati wa akifungua mkutano wa pili wa Mwaka wa wadau wa Mradi huo kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Katibu Mkuu wa wizara hiyo Dk.Leornad Akwilapo amesema benki ya Dunia imetoa Kiasi Dola za kimarekani Milioni 75 kwa ajili ya kutekeleza mradi huo katika vyuo vinne nchini ambavyo ni Chuo cha Usafirishaji Dar es Salaam (NIT), Taasisi ya Teknolojia ya Dar Es salaam (DIT) kampasi ya Dar es Salaam na Mwanza na Chuo cha Ufundi Arusha (ATC).
"Fedha hizi zinatolewa na Benki ya Dunia ni kwa ajili ya kuvijengea vyuo vya hivyo uwezo ili viweze kutoa wanafunzi wenye ujuzi stahiki wa kuwawezesha kujiajiri ama kuajiriwa na pamoja na kuvijengea vitu vya umahiri" amesema Dkt. Akwilapo.
Katibu Mkuu huyo ameongeza kuwa mradi huo utawezesha kujenga miundombinu bora na kuweka vifaa Pamoja na kuwajengea uwezo wakufunzi.
Aidha, Dkt. Akwilapo amewataka watanzania kufahamu kuwa elimu ya ufundi ni muhimu kwa maendeleo ya nchi hasa katika uchumi wa viwanda na kwamba vyuo vya ufundi visiwe chaguo la mwisho kwa mtu anayefeli.
"Tunawashukuru Benki ya Dunia kwa maana fedha hizo zitatumika katika kuhakikisha wanawajengea uwezo wanafunzi na pindi wanapohitimu inakua rahisi kuajiriwa viwandani na hasa ikizingatiwa Tanzania inaelekea katika uchumi wa viwanda kwa sasa,"
Naye Mratibu wa Mradi huo kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk.Noel Mbonde amesema vyuo hivyo vinne vimejikita katika masuala ya Teknolojia ya Habari(Tehama),Gesi asilia, Ngozi na masuala ya anga na mradi huo unakwenda kuongeza udahili wa wanafunzi katika fani hizo katika chuo cha NIT pamoja na ununuzi wa Ndege ya mafunzo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...



No comments:
Post a Comment