Search This Blog
Monday, November 25, 2019
Baraza la Biashara la Uholanzi-Afrika kunadi fursa za Uwekezaji
Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimetiliana saini makubaliano ya mashirikiano na Baraza la Biashara la Uholanzi-Afrika (NABC) hapo jana Novemba 25, 2019 katika Ofisi za TIC, Dar es Salaam.
Makubaliano hayo yamesainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Geoffrey Mwambe na Mkurugenzi Mkuu wa NABC Bw. Peter Ruiter na yamelenga kujenga mfumo wa pamoja wa kufanikisha biashara na uwekezaji zaidi baina ya Tanzania na Uholanzi.
Maafikiano ya makubaliano hayo ni matokeo ya mkutano uliofanyika kati ya TIC na NABC nchini Uholanzi, Februari, 2019.
NABC ina makampuni wanachama zaidi ya 300 ambayo yamewekeza katika sekta mbalimbali nchini Uholanzi na Sekta hizo ni pamoja na kilimo na kuongeza thamani, viwanda (nguo, maziwa), afya nishati, bandari, ujenzi, mifugo na kuongeza thamani.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment