Search This Blog
Saturday, October 5, 2019
Winga wa Juventus Douglas Costa Ampongeza mchezaji wa Simba
Winga wa miamba ya soka nchini Italia klabu ya Juventus, Douglas Costa amempongeza mchezaji wa Mabingwa wa tetezi wa ligi kuu soka Tanzania Bara Simba SC, Fraga Vieira kwa kuongeza mwaka mwingine katika siku yake ya kuzaliwa.
Kupitia akaunti yake ya Instagram, Douglas Costa amemtumia ujumbe mfupi beki huyo Simba baada ya kuweka picha yake ambayo akionekana akimwagiwa maji na wachezaji wenzake wa Msimbazi.
Douglas Costa de Souza akiwa na Ronaldo
Douglas Costa de Souza amempongeza nyota huyo kwa kuandika kuwa ”Caraleo, umekuwa ๐ด ! nakumbuka ukiwa chini ya miaka -15 Gerson ๐๐๐ hongera shujaa,” amesema mchezaji huyo wa Juventus.
Fraga Vieira raia wa Brazil amesajiliwa Simba SC akitokea katika klabu ya ATK FC ya India kwa mkataba wa miaka miwili.
Mchezaji huyo mwenye ambaye sasa anatimiza miaka 27 ana uwezo wa kucheza kama beki wa kati na kiungo mkabaji.
Vieira amewahi kuwa nahodha wa timu ya taifa ya Brazil ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 iliyokuwa na wachezaji maarufu kama vile Neymar, Philippe Coutinho na Casemiro.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment