Search This Blog
Saturday, October 5, 2019
Askari 6 Akiwemo wa JWTZ Wakuhumiwa kwa Wizi wa Mafuta ya Ndege
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu askari sita akiwemo Mwanajeshi wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) kulipa faini ya Sh 500,000 kila mmoja bada ya kukiri shtaka la wizi wa mafuta ya ndege (Jet A-1/Ik).
Askari hao ni Koplo Shwahiba(38), MT. 74164 SGT Ally Chibwana (47) wa JWTZ, PC Elidaima Paranjo (38), PC Simon (28), PC Dickson na PC Hamza Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi, Vick Mwaikambo baada ya Washtakiwa hao kukiri shtaka linalowakabili.
Mwaikambo alisema kwa kuwa Washtakiwa hao ni kosa lao la kwanza hivyo mahakama hiyo imewapa adhabu ya kulipa faini hiyo kila mmoja na madumu 109 yenye mafuta hayo yatarudishwa serikalini.
Awali wakili wa Serikali Mwandamizi Renatus alidai kuwa awali wastakiwa hao walikuwa wanakabiliwa na makosa matatu hivyo walikubaliana kuliondoa shtaka la kwanza la kupanga genge la uhalifu na shtaka la tatu ni la utakatishaji wa fedha na shtaka la pili la wizi limebaki.
Washtakiwa hao wanadaiwa kuwa Julai 30, mwaka huu katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere uliopo jijini Dar es Salaam, waliiba lita 2180 za mafuta ya ndege (Jet A-1/Ik) yenye thamani ya Sh 4,647,760 mali ya ATCL.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment