Search This Blog

Wednesday, October 16, 2019

Sehemu ya Bweni la Korogwe Girls lateketea kwa moto


Bweni la Shule ya Sekondari ya Wasichana (Korogwe girl) limeteketea kwa moto na kusababisha vifaa vya wanafunzi kuteketea kwa moto.

Kwa mujibu wa Mwalimu mkuu wa Shule ya Sekondari Korogwe girls, Anisia Mauka, moto huo umeteketeza sehemu ya bweni la Amani ambalo linatumiwa na wanafunzi wa kidato cha tatu na cha kwanza wakati wanafunzi wakiwa darasani wakijisomea.

Mwalimu huyo amesema, jumla ya vitanda 38 na magodoro yake pamoja na masunduku ya wanafunzi hao yameteketea kwa moto uliotokea jana usiku.

Chanzo cha moto huo bado hakijafahamika na hakuna vifo vilivyotokea isipokuwa kuna wanafunzi 12 ambao walipata mshtuko lakini wakapatiwa matibabu katika Hospitali ya Magunga na majengo na kwa sasa wanaendelea vizuri na wameruhusiwa.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...